Monday, November 26, 2012

Tusker Challenge Cup 2012 : Rwanda 2-0 Malawi , Zanzibar 0-0 Eritrea


Nahodha wa Rwanda, Haruna Niyonzima (katikati) akidhibitiwa na wachezaji wa Malawi, katika mchezo wa Kundi C, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge 2012 uliofanyika kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole, Kampala, Uganda usiku huu. Rwanda ilishinda 2-0, mabao ya Jean Baptiste Mugiraneza dakika ya 37 na Haruna Niyonzima dakika ya 79. 

Beki wa Zanzibar, Nassor Masoud ‘Chollo’, (kushoto) akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Eritrea, katika mchezo wa Kundi C, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole jioni hii. Timu hizo zilitoka sare ya bila kufungana.

No comments:

Post a Comment