Monday, July 17, 2023
Monday, July 10, 2023
MHE. BALOZI DKT. ELSIE KANZA AONGOZA SIKU YA MAADHIMISHO YA LUGHA YA KISWAHILI DUNIANI JIJINI WASHINGTON DC
Bendera zikiwakilisha mataifa ya Afrika ndani ya jengo la Ubalozi wa African Union Washington, DC, ambapo Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani uliadhimisha Siku ya Kiswahili Duniani, Ijumaa July 7, 2023 na Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Dkt. Elsie Kanza (hayuopo pichani ) aliongoza maadhimisho hayo. yaliyohudhuriwa na wadau mbalimbali wa lugha ya Kiswahili wakiwemo Waheshimiwa Mabalozi waalikwa pamoja na mwenyeji wao Balozi wa African Union nchini Marekani Mhe. Hilda Suka Mafudze. Picha na Vijimambo Blog |
Wa tatu toka kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Dkt. Elsie Kanza akiwa katika picha ya pamoja na wageni wake Mabalozi waalikwa. Wa kwanza kushoto ni Balozi wa Eswatini Mhe. Kennedy Fitzgerald Groening akifuatiwa na Balozi wa Ukraine Mhe. Oksana Markarova na wa mwisho kulia ni Balozi wa Kenya Mhe. Lazarus O. Amayo |
Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Elsie Kanza akiongoza maadhimisho ya siku ya lugha ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika siku ya Ijumaa July 7, 2023 katika jengo la Ubalozi la African Union Washington, DC. |
Balozi wa African Union nchini Marekani Mhe. Hilda Suka Mafudze (kulia) akitoa hotuba ya ufunguzi siku ya maadhimisho ya lugha ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika katika jengo la Ubalozi la African Union Washington, DC. Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Dkt Elsie Kanza akifuatilia hotuba hiyo. |
Watatu toka kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Dkt Elsie Kanza akiwa na wageni wake waheshimiwa Mabalozi walioalikwa kuhudhuria maadhimisho ya siku ya lugha ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika siku ya Ijumaa July 7, 2023. Washington, DC. |
Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Dkt Elsie Kanza akiwa na wageni wake waheshimiwa Mabalozi walioalikwa kuhudhuria maadhimisho ya siku ya lugha ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika siku ya Ijumaa July 7, 2023. |
Wadau wa lugha ya Kiswahili wakifuatilia maadhimisho hayo yaliyofanyika siku ya Ijumaa July 7, 2023 katika jengo la Ubalozi la African Union lililopo Washington, DC nchini Marekani. |
Monday, June 26, 2023
Tuesday, June 20, 2023
UKODAK MOMENT OLD SCHOOL REUNION DMV SIKU YA IJUMAA
Kushoto ni Dj Dennis Shengena kutoka Minnesota akiwa sambamba na Dj Rexx kutoka Houston, Texas wakiwasha moto Karibu Night iliyofanyika siku ya Ijumaa June 16, 2024 Silver Spring, Maryland katika kiota cha Hakuna Matata Grill, huu ulikua usiku wa kwanza wa Old school reunion iliyokutanisha wadau mbalimbali kutoka kila pembe ya USA na sehemu nyingine Duniani. Picha na Vijimambo Blog. |
Wadau wakifurahia muziki kutoka kwa Dj Dennis Shengena na mshirika wake Dj Rexx kutoka Houston, Texas |
Papa Kinyasi akiburudika na kanywaji huku akipunga upepo mwanana |
JUMAMOSI YA OLD SCHOOL REUNION YABAMBA
Dj Dennis Shengena (kushoto mwenye suti ya blue) akiwarusha wadau waliofika DMV kutoka kila pembe ya USA na Duniani kote, kulia ni NY Ebra akifurahia jambo na Dj Dennis, nyuma ni Dj Musmus ambaye alikuwa mshereheshaji wa usiku huo uliofanyika West Bowie Village Hall, Bowie Maryland nchini Marekani, Jumamosi June 17, 2023. Picha na Vijimambo Blog |
Dj Musmus kutoka Michigan akipata ukodak moment |
VIVAZI VILIVYOTAMBA OLD SCHOOL REUNION ZULIA JEKUNDU JUMAMOSI DMV
Wapili toka kushoto ni msanii wa kizazi kipya Roma Mkatoliki akiwa na mchekeshaji Beneficial (watatu toka kushoto) kwa pamoja wakipata picha na wadau waliokua nao siku ya Old School Reunion iliyofanyika Jumamos June 17, 2023 Bowie, Maryland nchini Marekani. Picha na Vijimambo Blog. |
Dj Dennis akipata ukodak moment zulia jekundu |
Ndaga Mwakabuta toka Minnesota akipata picha katika zulia jekundu |
Catherine Shirima na Ndaga Mwakabuta katika picha ya pamoja |
Catherine Shirima na Dj Dennis katika picha ya pamoja |
Amina Ibuni akiwa katika zulia jekundu |
Subscribe to:
Posts (Atom)