Tuesday, October 1, 2024

DIASPORA WA MAREKANI WAJITOKEZA KWA WINGI KUSHUGHULIKIA PASI ZA KUSAFIRIA NA VITAMBULISHO VYA NIDA

 Afisa uhamiaji Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Bi Sophia Gunda akihakiki karatasi za mmoja ya wadau wa Diaspora aliyafika Austin, Texas kushughulikia swala la pasi ya kusafiria siku ya Jumamosi Septemba 28, 2024. Picha na Vijimambo Blog

Afisa uhamiaji Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Bi Sophia Gunda akihakiki karatasi za mmoja ya wadau wa Diaspora aliyafika Austin, Texas kushughulikia swala la pasi ya kusafiria siku ya Jumamosi Septemba 28, 2024.
Afisa usajili mwandamiz Issa Salumi akihakiki maelezo ya diaspora mTanzania nchini Marekani yanasomeka kama yalivyojazwa kwenye fomu za mwombaji wa kitambulisho cha NIDA.
Kushoto ni Theresia Matonya afisa uchambuzi mifumo ya kompyuta akihakiki fomu za mmoja ya waombaji wa kitambulisho cha Taifa (NIDA)
picha juu na chini ni Afisa uhamiaji Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Bi Sophia Gunda akihakiki karatasi za mmoja ya wadau wa Diaspora aliyafika Austin, Texas kushughulikia swala la pasi ya kusafiria siku ya Jumamosi Septemba 28, 2024.
Kwa picha zaidi bofya soma zaidi

BALOZI WA TANZANIA NCHINI MAREKANI NA MEXICO, MHE. DKT. ELSIE KANZA ATEMBELEA MEZA ZA WAJASIRIAMALI WAKIWEMO WADAU WA UTALII WALIOHUDHURIA KONGAMANO LA DIASPORA, AUSTIN, TEXAS

Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico akipata picha ya kumbukumbu mara tu baada ya kuwasili kwenye kongamano kubwa la Diaspora lililofanyika kwa siku 3 Austin, Texas nchini Marekani. Picha na Vijimambo Blog
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo,akiwasili kwenye kongamano akiongozana na afisa Ubalozi Abdul Malik (kulia) siku ya Jumamosi Septemba 28, 2024 Austin, Texas kwenye resort ya Kalahari.
Watatu toka kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo akiwa na mwenyeji wake, Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Dkt. Elsie Kanza wakiwa katika picha ya pamoja na wadau wa wa Bank ya NMB mara tu walipowasili kufunga kongamano kubwa la Diaspora lililofanyika kwa siku 3 Austin, Texas nchini Marekani siku ya Jumamosi Septemba 28, 2024.
Mmoja ya mdau waliohudhuria kongamano la Diaspora nchini Marekani akipata picha na  Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Dkt. Elsie Kanza
 Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Dkt. Elsie Kanza akiwa na mgeni wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo wakipita kwenye meza za wajasiriamali na wadau wa utalii waliokuja kwenye kongamano kubwa la Diaspora nchini Marekani lililofanyika Austin, Texas katika Reosort ya Kalahari,
Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Dkt. Elsie Kanza akisalimiana na wadau kutoka Vodacom alipotembelea meza yao.
Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Dkt. Elsie Kanza akisalimiana na wadau kutoka Vodacom alipotembelea meza yao.
Mmoja ya mdau akikabidhi kitabu  alichoandika kwa Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Dkt. Elsie Kanza 
Kwa picha zaidi bofya soma zaidi

BALOZI WA TANZANIA NCHINI MAREKANI NA MGENI WAKE WAZIRI WA OFISI YA RAIS MIPANGO NA UWEKEZAJI WAKIWA WAGENI WA HESHIMA MTANANGE WA SIMBA NA YANGA AUSTIN, TEXAS.

 Mtanange wa Simba na Yanga Austin, Texas umeisha kwa Yanga kufungwa kwa taaabu na Simba. Kipindi cha kwanza Simba ilitangulia kwa kupata mabao mawili ya haraka yaliyofungwa na James Kittilya dakika ya 2 tu ya mchezo na la pili lilifungwa na Micky JR dk ya 35 ya mchezo. Yanga walichangamka dakika ya 36 na kupata bao la penalty kupitia kwa nyota wao kijana Ally Ngolo na dakika chache kabla ya mapumziko walipata bao la kusawazisha kupitia kwa mshambiliaji wao Richard Mbappe ingawa mfungaji alikuwa ameotea lakini refa Ricky Reynolds maarufu kama Bongozozo Timu ya Yanga walimtilia mashaka refa Bongozozo baada kujisahau na kushangilia goli alilofunga mwanae Micky. Ukiondoa kasoro hii refa aliweza kubalansi mchezo.


 Kipindi cha pili Simba waliingia kwa nguvu na kupata mabao matatu ya haraka yaliyofungwa na Kelvin Onesmo dk 48, Kisuby Warro dk ya 64 na Justice Munissi dakika ya 72 kabla yanga hawajapata bao la tatu kupitia kwa Ally Ngolo tena dk ya 86. Hadi muamuzi anapuliza filimbi ya mwisho Simba 5-3 Yanga. Mgeni rasmi alikabidhi kombe la DICOTA CONVENTION CUP kwa msimu wa 2024-2025 kwa kocha/mchezaji wa Simba Maestro Cassius Pambamaji na kuanzisha shangwe na nderemo kutoka kwa mashabiki wa timu zote mbili. *video ni Simba wakikabidhiwa kombe lao na wachezaji na mashabiki wakishangilia* Tukutane msimu ujayo Yanga wajipange vizuri
Mhe. Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Dkt. Elsie Kanza akiwa na mgeni wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, wakiwasili uwanjani kushuhudia mtanange wa watani wa jadi, Simba vs Yanga mechi iliyofanyika siku ya Jumampso Septemba 28, 2024 Austin, Texas na  Simba kuibuka na ushindi wa 5G zidi ya Yanga.Picha na Vijimambo Blog.
Kulia ni wawakilishi wa CRDB ambao walidhamini jezi na kombe kwenye mechi hiyo ya Simba na Yanga
Kepteni wa Yanga Eddie akikabidhiwa jezi ya Yanga na mdhamini CRDB
Kepteni wa YangaCassihno akikabidhiwa jezi ya Simba na mdhamini CRDB
Mhe. Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Dkt. Elsie Kanza akisalimiana na Haji Manara  semaji la Yanga Marekani kabla ya mechi wakati wa Mhe. Balozi na mgeni wake walipokua wakisalimiana na wachezaji.
Mhe. Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Dkt. Elsie Kanza akiwa na mgeni wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo wakiongea jambo na Bongo Zozo kabla ya zoezi la ukaguzi wa timu mbili.
Mhe. Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Dkt. Elsie Kanza akiwa na mgeni wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo wakiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa Simba,
Mhe. Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Dkt. Elsie Kanza akiwa na mgeni wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo wakiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa Yanga.
Kwa picha zaidi bofya soma zaidi

WADAU WA UTALII WAKUTANA FARAGHA KWENYE KONGAMANO LA DIASPORA AUSTIN, TEXAS

 

Jopo la utalii likiongoza kikao na wadau wa utalii na kutoa elimu ya njia mbalimbali za  jinsi ya kukuza utalii Tanzania. Kikao hicho kilitenga chumba maalum kuzungumzia swala hilo siku ya Jumamosi Septemba 28, 2024 Austin, Texas kwenye resort ya Kalahari. Picha zaote na Vijimambo
Wadau wa utalii wakifuatilia kikao.