Friday, September 12, 2014

Mhe.Lazaro Nyalandu awasili kuhudhuria Tamasha la Utalii na Miaka 4 ya VIJIMAMBO

Mhe. Lazaro Nyalandu, Waziri wa Maliasili na Utalii akipokewa na Afisa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani, Suleiman Saleh mara tu alipowasili katika uwanja wa kimataifa wa Dulles kwa ajili ya kuhudhulia tamasha la Utalii na miaka 4 ya Blog ya Vijimambo litakalo fanyika Jumamosi Sept 13, 2014. Kushoto ni msaidizi wa Waziri Bwn. Iman Nkuwi.
 
Msanii wa kizazi kipya Cassim Mganga akipiga picha na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Lazaro Nyalandu walipokutana kwenye jengo la Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani ulipo jijini Washington, DC.
 Msanii wa kizazi kipya Cassim Mganga akipata picha za kumbukumbu nje ya mjengo wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani
 Cassim Mganga akipata picha ya pamoja na Afisa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani Bwn. Swele.
 Msanii wa Bongo Flava Cassim Mganga akipata picha ya pamoja na wadau wanao tangaza Utalii wa Tanzania nchini Marekani.
 Cassim Mganga akisalimiana na Mhe. Liberata Mulamula Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani.
 Mwanamuziki wa kizazi kipya Cassim Mganga akipata picha ya kumbukumbu na Mwambata wa jeshi Ubalozi wa Tanzani nchini Marekani na Canada, Clonel Adolph Mutta.
 Mwanamuziki wa kizazi kipya Cassim Mganga akipata picha ya kumbukumbu na Aunty Mercy Dachi.

No comments:

Post a Comment