Thursday, February 12, 2015

Mauaji ya wanafunzi waislamu yazua hisia

 
Maafisa wa polisi mjini NORTH Carolina nchini Marekani wamemkamata mtu mmoja baada ya wanafunzi watatu waislamu kupatikana wamefariki nyumbani mwao.
 
 
Miili ya Deah Barakat,mkewe Yusor Mohammed Abu salha na dadaake Razan Mohammed Abu salha ilipatikana siku ya jumanne ikiwa na majeraha ya risasi katika vichwa .

Mtu mmoja mwenye umri wa miaka 46 tayari amefunguliwa mashtaka kutokana na mauaji hayo.

Maafisa wa polisi wanasema wanajaribu kubaini iwapo mauaji hayo yanatokana na chuki.

Swala kwamba wanafunzi waliouawa ni waislamu limezua uvumi katika mitandao ya kijamii wa iwapo mauaji hayo ni ya kidini au la

Uchunguzi uliofanywa umebaini kwamba uhalifu huo ulitekelezwa kutokana na mzozo unaondelea kuhusu uegeshaji wa magari,maafisa wa polisi wa Chapell wamesema.

No comments:

Post a Comment