CHELSEA WAGONGA MWAMBA UJERUMANI, WENGER AENDELEA KUSAJILI MAKINDA
Tetesi za J'tatu magazeti ya Ulaya
KLABU ya Bayer Leverkusen
imeitupilia mbali ofa ya Chelsea kwa mshambulaji wao mwenye umri wa miaka 21,
Andre Schurrle.
KOCHA
Alan Pardew amesema kwamba anafanya kila atakachoweza kuhakikisha anambakiza
mshambuliaji Demba Ba, mwenye umri wa miaka 27, katika klabu ya Newcastle.
Spurs inamtaka Daniel Sturridge |
TOTTENHAM
Hotspur inataka kutoa dai la pauni Milioni 5 kumsajili mshambuliaji mwenye umri
wa miaka 22, Daniel Sturridge wa Chelsea.
KIUNGO
wa Arsenal, Aaron Ramsey, mwenye umri wa miaka 21, amesema kwamba yeye na
wachezaji wenzake hawajui mambo yatakuwaje mshambuliaji wao Robin van Persie
akiondoka.
KOCHA
wa Swansea City, Michael Laudrup anajaribu kumsajili winga wa Bristol City,
Albert Adomah kutoka Ghana mwenye umri wa miaka 24, usajili ambao unaweza
kumgharimu pauni Milioni 3.
KOCHA
Roberto Mancini yupo karibu kusaini mkataba mpya na Manchester City, licha ya
Chama cha Soka Urusi kutenga kitita kizito kujaribu kumnasa.
KLABU
ya Liverpool imekula za uso tena, baada ya kukataliwa kuuziwa kiungo mwenye umri
wa miaka 25, Esteban Granero na Real Mdrid.
KLABU
ya AC Milan imesema ni bora kumchukua kwa mkopo kuliko kumnunua jumla
mshambuliaji wa Liverpool, Andy Carroll, mwenye umri wa miaka 23.
KLABU
ya Fiorentina inamtaka mshambuliaji wa kimataifa wa Morocco, Marouane Chamakh,
mwenye umri wa miaka 28, ambaye anajiandaa kuondoka Arsenal baada ya mambo
kumuendea ovyo.
KOCHA
wa Wigan, Roberto Martinez anamtaka winga wa Chicago Fire, raia wa Guatemala,
Marco Pappa, mwenye umri wa miaka 24 azibe nafasi ya mchezaji anayetakiwa na
Chelsea, Victor Moses.
KLABU
ya Arsenal nayo ipo kwenye mkakati wa kumnunua mchezaji wa Wigan, Victor
Moses, mwenye umri wa miaka 21.
KLABU
ya Norwich imetoa ofa kwa ajili ya mshambuliaji wa Canaries, James Vaughan,
mwenye umri wa 23, kwa Birmingham kuwasaidia kumbakiza beki wa kati, Curtis
Davies, mwenye umri wa miaka 27.
KIKOSI
cha Tottenham Hotspur sasa kipo kamili chini ya kocha mpya, Andre-Villas Boas,
kwa mujibu wa Danny Rose, mwenye umri wa miaka 22.
KOCHA
Roberto Mancini aliepuka mapokezi wakati kikosi cha Manchester City kilipowasili
katika kambi yao ya kujiandaa na msimu mpya nchini Austria, kulingana na tetesi
zinazozagaa kuhusu mustakabali wake.
MSHAMBULIAJI
wa Manchester City, Edin Dzeko ameungana na mwigizaji nyota wa Hollywood,
Angelina Jolie katika zuli jekundu kwenye tamasha la filamu mjini
Sarajevo.
No comments:
Post a Comment