Meli ya Mv Skagit iliyokuwa safarini kutoka Dar kuelekea Zanzibar
imezama majira ya saa nane mchane hivi leo katika maeneo Pungume na
Chumbe baada ya kukumbwa na upepo mkali.
Meli hiyo inayosadikiwa kuwa na abiria 250 inasemekana imepindukia
upande mmoja na huku abiria wengi wakiweza kuokolewa kutokana na
jitihada mbali mbali kupitia vile vile msaada wa boti za Mv Kilimanjaro,
Tug ya Bandari na vyombo vyengine.
Mpaka tunandika taarifa hizi ni maiti tatu zilikwishapatikana na
kiasi cha abiria 150 wameokolewa na waliojeruhiwa wanatibiwa
katika Hospitali ya Mnazimmoja. Taarifa zinaeleza kwamba
kulikuwa na watoto takriban 30 na Watalii kutoka nchi mbali mbali
wafikao kumi.
Wazamiaji kutoka Kikosi cha KMKM pamoja na Jeshi tayari wapo
eneo la ajali kusaidia kuokoa maisha ya wananchi waliokumbwa
na maafa haya.
Majeruhi alieokolewa
katika meli ya StarGate
iliozama huko katika bahari
ya Chumbe Zanzibar na
ikiwa na abiria 250.
No comments:
Post a Comment