Saturday, July 14, 2012


SIMBA WAFIKIRIA KUJITOA KAGAME

Yondan anasaini Yanga na mpunga mezani huo

Simba SC wapo kwenye kikao kujadili juu ya uamuzi wa kushiriki au kutoshiriki 
mchuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, maarufu kama Kombe la Kagame,
 iliyoanza leo Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam.

Kisa nini? Hawana imani na wenyeji wa michuano hiyo, Shirikisho la Soka 
Tanzania (TFF) pamoja na Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na 
Kati (CECAFA). Kivipi? Ni kutokana na kitendo cha vyombo hivyo kumpa
 leseni beki wao  Kelvin Patrick Yondan achezee Yanga SC, ambao ni wapinzani 
wao wa jadi.

Habari ambazo BIN ZUBEIRY imezipata kutoka ndani ya Simba SC, zimesema
 kwamba kitendo cha Yanga kumchezesha Yondan kwenye klabu hiyo leo, katika 
mchezo dhidi ya Atletico ya Burundi, kimeikera sana Simba na kinahisi kuna 
hujuma wanafanyiwa na TFF na CECAFA.

Ikumbukwe Yondan aliyejiunga na Simba 2006, alijiunga na Yanga mwezi
 uliopita ingawa klabu yake inaendelea kudai, ina mkataba naye.
BIN ZUBEIRY ilifanikiwa kuwa chombo cha kwanza cha habari duniani
 kuonyesha mikataba yote ya Simba na Yanga dhidi ya Yondan.

Lakini Yondan beki wa kati hodari nchini, mwenyewe hajawahi hata siku 
moja kuukana mkataba wowote kati ya hiyo, zaidi ya kusema kujiunga kwake 
na Yanga, Simba watajijua wenyewe.


Mwishoni mwa mwaka jana, Yondan alisusa kuchezea Simba na kuamua 
kubaki kwao mjini Mwanza, baada ya mechi dhidi Toto African ya mini humo
 ya Ligi Kuu.

Na ndipo hapo zilipoanza kuibuka habari za mchezaji huyo kuhamia kwa watani
 wa jadi, hadi Mei mwaka huu alipomwaga wino Jangwani. Ingawa Yondan kwa 
sasa yupo kwenye kambi ya timu mpya ya Yanga, lakini klabu yake Simba SC
 imeendelea kusiistiza huyo ni mchezaji wao halali na sasa inafikiria kujitoa
 kwenye Kagame baada ya Vidic wa Tanzania kuchezea Yanga kwenye 
michuano hiyo.    

No comments:

Post a Comment