Saturday, July 14, 2012


SOCCER: Wichita FC vs Houston FC in Wichita!!!!!PDFPrintE-mail
  
2012 Soccer
Wichita FC vs Houston FC in Wichita

Ile Timu yenu ya mahiri ya soka, Wichita FC iliyokuwa imeweka kambi kabambe nje kidogo 
ya mji, inafuraha kuwatangazia kwamba imerudi mafichoni na inakukaribisha kushuhudia
 kabumbu la hali ya juu wakati watakapowakaribisha mahasimu wao wa jadi kutoka Houston


 TXJumamosi July 14 kwenye uwanja wa Stryker Soccer Complex (Greenwich & 29 Address: 
2999 N. Greenwich Rd. Wichita, KS 67226) kuanzia kumi na mbili unusu jioni kwa saa 
za Wichita(6:30pm CT)
Meneja wa Timu Mazaza Wa Mtawali (aka B.I.G) anaripoti vijana wake wapo fiti, wenye afya 
njema na nidhamu ya hali ya juu. Mazaza anasema anawakati mgumu sana mwaka huu wa 
kupanga kikosi kitakachovalia uzi wa kuichambua Houston kutokana na uchu walioonyesha
vijana wakati wa maandalizi ya mechi hii. Kapteni wa Wichita FC Diwani Cheche ameahidi 
ushindi mnono na kuundeleza uteja wa Houston FC mbele ya vijana wa Wichita.
TaWichita inawakaribisha kwa moyo mkunjufu wa "Mgeni Njoo..." ndugu zetu wa Houston FC, 
na wapemichezo wote wa Wichita na vitongoji vyake kwenye "shughuli" hii kati ya mwezi huu. 
Tunauhakika Wichita FC litaibuka kidedea, kama kawa!

No comments:

Post a Comment