Sunday, December 8, 2013

NEW YORK TANZANIA TEAM YAIANGUSHIA KIPIGO TIMU YA BOSTON 7 KWA 3

Mh. Balozi Manongi akisalimiana na wachezaji wa timu ya Umoja New England Boston kabla ya mpambano wa kukata na shoka. Timu ya watanzania New York ilipata nafasi ya kuonyesha makucha yake baada ya mazoezi yaliyochukua takribana miezi 4.  Boston walikuja kukata mzizi wa fitina baada ya majigambo ya muda mrefu matokeo yake walikutana na kipigo cha mbwa mwizi kwa kunyukwa bao 6 kwa 3.
 Mh. Balozi akisalimiana na wacheza wa New York kabla ya mchezo huo wa kuka na mundu, mchezo ulikuwa mzuri na kila timu ilionyesha mchezo wa kuvutia lakini ni New York ikiwatumia vijana wake wanye vipaji ilifanikiwa kuizima Boston kila idara.

 Kocha wa New York Tanzania Team Salim Akida akifurahia ushindi wa timu yake akiwa na Mh.Balozi Manogi na Captain wa Team Muba.
 Picha ya pamoja wachezaji na viongozi wa timu kabla ya mchezo
 Mambo yalikuwa kama hivi vijana wakifanya vitu vyao uwanjani
 Mh. Balozi Mwinyi akiwa na vijana wake uwanjani hapo, vijana hawa wa Mh ni moja ya vipaji vya Timu ya New York.
Mpira ukiwa nyavuni kuandika bao la 6 bao lilifungwa na capatin wa timu Muba kutoa umbali wa nusu ya uwanja.

No comments:

Post a Comment