Sunday, February 9, 2014

Mdahalo wa wagombea Uongozi TZ-Houston Community wafanyika Houston

Jumuiya ya Watanzania waishio katika jiji la Houston, Texas jioni ya leo imefanya mdahalo wa wagombea nyadhifa za Uenyekiti na Ukatibu mkuu wa jumuiya katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu.Nafasi ya mwenyekiti inagombewa na Bw.Issa Kingu, Bw.Erasto Mvungi, Bi.Nuru Mazora na Bw.Isaiah Mgendi.Wakati nafasi ya Ukatibu inagombewa na katibu anayemaliza muda wake Bi.Leyla Kikuzi na Bw.Alfred Nkunga.

Mdahalo huo ulioandaliwa na Kamati ya Uchaguzi chini ya Mwenyekiti wake Bw.Steve Maonyesho na kuendeshwa na Bw.James Shemdoe (Moderator) ulihudhuriwa na idadi ya kuridhisha ya Watanzania waishio katika jiji hilo la Houston na kurushwa live kupitia mtandao kwa wale ambao hawakuweza kuhudhuria. Zifuatazo ni picha za tukio hilo. 

Wagombea nafasi ya Mwenyekiti toka kushoto Bw.Mgendi , Bw.Mvungi na Bw.Kingu

Moderator wa Mdahalo Bw.Shemdoe
Bw.Nkunga akiuza sera 

Wagombea

Shughuli inaendelea

Sehemu ya wanajumuiya wakisikiliza sera za Wagombea

Bi.Leyla akimwaga sera



Cameraman Bw.Fue

Dk.Tenende akifuatilia mdahalo kwa makini

Maswali yakiendelea kuulizwa


Wagombea
Bw.Mgendi akimwaga sera

Wenye Jumuiya yao





Mwenyekiti wa kamati ya Uchaguzi Bw.Maonyesho
Mwenyekiti anayemaliza muda wake Bw.Novatus Simba akichangia

Dk.Tenende na Bw.Andrew Sanga


No comments:

Post a Comment