Monday, December 6, 2021

KAMATI YA MIJI DADA YA DURHAM NA ARUSHA WAMKARIBISHA BALOZI ELSIE KANZA KWENYE MIAKA 60 YA UHURU NA USHIRIKIANO WA TANZANIA NA MAREKANI

Picha juu na chini ni Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani
Mhe. Elsie Kanza akitoa neno la shukurani kwa kamati ya miji dada Durham na
Arusha kwa kumkaribisha kwenye maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara na
 kuahidi kutoa ushirikiano kwa kamati hiyo katika kuendelezamashirikiano kati ya nchi za Tanzania
 na Marekani katika nyanja mbalimbali za maendeleo ikiwemo uwekezaji.
Picha na Vijimambo Blog


Mwenyekiti Mwenza wa kamati ya miji dada Durham na Arusha (SCD)
Bi. Ronda Pierce akieleza historia ya kamati ya miji dada na mashirikiano yao na mji
wa Arusha na Durham tangu mashirikiano hayo yalipoanzishwa.

Meya wa mji wa Durham anaemaliza muda wake Bw. Steve Schewel akimkaribisha Balozi
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Elsie Kanza na
kuelezea mashirikiano ya mji wa Durham na Arusha na safari yake nchini Tanzania
hususani kwenye mji wa Arusha.

Rais wa miji dada ya Durham na Arusha (SCD) Bwn.Tom Harris akitoa salamu kwa
Mhe. Balozi kutoka kwa Kamati ya miji dada ya Durham na Arusha (SCD)

Kansela wa Chuo Kikuu cha NCCU ( North Carolina Central University) Bwn. Jonson
Akinleye akimkaribisha Mhe. Balozi na kamati ya miji ya Durham na Arusha chuoni hapo
 siku ya Jumapili Disemba 5, 2021 siku SCD walipomkaribisha Balozi kwenye maadhimisho
ya miaka 69 ya Uhuru wa Tanzania Bara.

Mwenyekiti Mwenza wa Kamati ya miji ya Durham na Arusha Bi.Gwendolyn Bookman
akitambulisha Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani,
Mhe. Elsie Kanza kwa kusoma wasifu wake na baadae kumkaribisha kuongea na
hadhara iliyojumuika pamoja na kamati ya miji dada ya Durham na Arusha katika
maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara

Picha juu na chini ni Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani
Mhe. Elsie Kanza akipokea zawadi mbalimbali kutoka kwa Meya wa Durham anayemaliza
muda wake akiwemo Rais wa SCD (miji dada ya Durham na Arusha) na wadau wengine
kwenye maadhimisho hayo ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara.





Meya mteule wa Durham Bi. Elaine Neel akiwa katika picha ya pamoja na
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Elsie Kanza

Meya wa zamani wa mji wa Durhan Mhe.William Bell akiwa katika picha ya pamoja na
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Elsie Kanza

Kansela wa Chuo Kikuu Cha NCCU ( North Carolina Central University Bwn. Johnson Akinleye
akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini
Marekani Mhe. Elsie Kanza

Mwenyekiti wa Jumuiya ya waTanzania North Carolina Scolastica akiwa katika picha
ya pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani
Mhe. Elsie Kanza

Kushoto ni Afisa Ubalozi Bi Jean Msabila na Mkuu wa Utawala na Fedha Bi. Eva Ng'itu
wakifuatilia jambo kwenye maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara
yaliyokuwa yameandaliwa na Kamati ya Miji dada ya Durhan na Arusha katika Chuo Kikuu
cha NCCU (North Carolina Central University) siku ya Jumapili Disemba 5, 2021.

Picha juu na chini wageni waalikwa wakiwemo wadau mbalimbali wakifuatilia
maadhimisho hayo.








Picha juu na chini wadau mbalimbali wakiuliza maswali wakiwemo wawekezaji wanaowekeza
 nchini Tanzania wanaotokea North Carolina.







Picha juu na chini wageni waalikwa wakiwemo wadau wakibadilishana mawili matatu
kabla ya maadhimisho hayo ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara kuanza.




No comments:

Post a Comment