Saturday, March 10, 2012

YANGA YACHAPWA MAGOLI 3-1 NA AZAM FC, MAKONDE YATEMBEA

Mwamuzi Israel Mkongo pamoja na wasaidizi wake akitoka nje kwa kusindikizwa na askali wa kikosi cha kutuliza Ghasia FFU mara baada ya kupuliza kipenga cha mwisho kwenye mchezo wa ligi kuu ya Vodacom uliokutanisha timu ya Yanga ya Jangwani na timu ya Azam FC kutoka Chamazi ambapo Yanga imekandamizwa magoli 3-1 na wauza Sembe hao wa Chamazi kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Mwanzo ulikuwa ni mchezo mzuri uliokuwa wa vuta nikuvute kwa kila upande lakini mambo yalibadilika mara baada ya Azam kuandika goli la kwanza, mchezaji Haruna Niyonzima wa Yanga alionekana kumlalamikia refa mara kwa mara jambo ambalo refa alimuonya mara kadhaa lakini, hata hivyo Niyonzima aliendelea baada ya muda, alitolewa nje kwa kadi nyekundu, jambo ambalo lilizua tafrani uwanjani huku makonde yakirushwa hovyo, baadae naye mchezaji Nadir Haroub Canavaro alipewa kadi nyekundu kutokana na vurugu hizo na kuzua tifu lingine uwanjani. Hali ilikuwa kama hivi angalia matukioo ya picha hizi.
Canavaro akitolewa nje huku huku akilia na kocha wake Papic akimtuliza.
Papic akiwatuliza wachezaji na baadhi ya maafisa wa benchi la ufundi
Canavaro akizuiwa na wenzake asimshushie kipondo refa huyo.
Polisi akiwa ameingia uwanjani ili kutuliza fujo hizo na kutoa ulinzi kwa refa huyo.
Mchezaji John Boko wa Azam FC akimtoka beki wa Yanga Haroub Nadir Canavaro.
Mashabiki wa Azam FC wakishangilia kwa furaha.
John Boko akishangilia mara baada ya kuipatia timu yake goli la kwanza.
Timu zikiingia uwanjani tayari kwa kuanza mchezo huo leo.

No comments:

Post a Comment